Lorem ipsum dolor sit amet
consectetur. Non molestie.
Lorem ipsum dolor sit amet
consectetur. Non molestie.
Lorem ipsum dolor sit amet
consectetur. Non molestie.
Lorem ipsum dolor sit amet
consectetur. Non molestie.
Mkakati wa kidijitali wa waleta mabadiliko unatambua na kusaidia wajasiriamali kijamii wa ndani kwa masuluhisho ya ubunifu ambayo yanalenga kuibadilisha jamii kwa kutumia programu/teknolojia za kidijitali. Tangu kuanzishwa kwake mwaka 2012 kama Tigo Reach for Change na baadae kubadilishwa kuwa Digital Changemakers mwaka 2014 tumeshaweza kuwavutia na kuchagua masuluhisho muhimu ambayo yamekuwa na matokeo chanya kwa watoto na jamii kwa jumla.
Tumewekeza kwa watu binafsi ambao wanavutia kwa matokeo, wanapenda na wana sifa za kiujasiriamali na kuwapatia programu muhimu zinazohitajika katika ubunifu wa suluhisho la matatizo yanayoikabili jamii. Digital Changemakers wanapewa msaada wa fedha na ufundi kupitia kituo chetu cha mfano na wanaunganishwa na washauri na wataalamu wa Tigo katika kuwasaidia na kuendeleza miradi yao. Ifuatayo hapa chini ni orodha ya Changemakers wetu ambao wameshaweza kuleta mabadiliko kwa watoto 15,000 katika maeneo tofauti kupitia miradi yao.
CAROLYNE EKYARISIIMA – APPS & GIRLS
Akiwa amelenga kuziba pengo la kijinsia katika Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama) nchini Tanzania, Carolyne anaendesha programu yake ya Apps & Girls ambayo inahamasisha na kuwezesha watoto wa kike walio na umri wa miaka 10 hadi 18 kujifunza kompyuta na kuanzisha ubunifu wa kidijitali. Kwa kuanzisha klabu maalumu katika mashule na kupitia matukio ya kama vile warsha, maonesho, kuweka makambi na mashindano asasi hii inaunda viongozi wanawake wa baadaye nchini Tanzania. Kwa taarifa zaidi tembelea: http://www.appsandgirls.com/
BRENDA SHUMA – GABRIELLA CENTRE
Akiwa amehitimu katika Chuo Kikuu cha Tumaini katika shahada ya therapia ya viungo, Brenda-Deborah Shuma ambaye muasisi wa kituo cha Gabriella Children Rehab amewekaza muda na elimu yake katika kuwalea watoto walio na mtindio wa ubongo pamoja na uoni hafifu. Brenda alishafanya kazi na Kituo cha YWCA Children Rehabilitation, ambapo alishiriki katika kuunda na kuanzisha wiki ya programu ya kina ya therapia kwa watoto walio na ulemavu. Ni mapenzi haya pamoja na uzoefu uliomshawishi kufungua kituo cha Gabriella Children Rehab mjini Moshi Tanzania. Kwa taarifa zaidi tembelea: http://www.gabriellarehab.org
FARAJA NYALANDU – SHULE DIRECT
Faraja ni mwanasheria, mwenye mapennzi katika kuhamasisha na kushughulikia haki za kijamii za watu. Anapendelea masuala yanayohusu haki za watoto, elimu bora, kuwezesha wanawake na haki za binadamu. Ni muasisi mwenza wa Shule Direct ambao ni ujasiriamali jamii ukijielekeza kushughulikia kukabili ukosefu wa vitabu vya kutosha katika shule za sekondari kwa kukusanya mada nzuri kutoka kwa walimu wenye sifa na kuzifanya kupatikana bure kupitia mtandao.asasi hivyo inatoa fursa kwa wanafunzi nchini Tanzania kujifunza na kutambua umuhimu wao. Kwa taarifa zaidi: www.shuledirect.co.tz/
JOAN AVIT- GRAPHOGAME TANZANIA
Kujifunza kusoma ni jambo muhimu katika uelewa, ubora wa elimu na kutokomeza umasikini. Hata hivyo takribani theluthi mbili ya watoto nchini Tanzania hadi kufikia darasa la pili wanakuwa hawana uwezo wa kusoma! Joan Avit kupitia mradi wake Graphogame Tanzania ameanzisha mbinu ya kufundisha kidijitali ambayo inatumia mchezo katika simu ya mkononi na kufundisha watoto wadogo kusoma katika maeneo ya vijijini mkoani Kilimanjaro. Kwa taarifa
zaidi: http://info.graphogame.com/
THADEI MSUMANJE – MAJENGO KIDSYOUTH & TECHNOLOGY SCHOOL
Thadei Msumanje anaamini kwamba teknolojia ni programu yenye nguvu katika maendeleo ambayo inaweza kutumiwa kuendeleza elimu duniani, maisha pamoja na afya. Kupitia asasi yake ya Majengo Kids Youth & Tech School, analikabili tatizo hili kwa kuileta teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama) kwa watoto ndani ya jumuiya za vijijini. Amejumuisha kujifunza Tehama na miundo mingine ya kujifunza kama vile shule za awali kwa kuhakikisha kwamba faida za Tehama katika hatua za kujifunza zinapatikana kwa watoto wote katika maeneo ya vijijini Tanzania.
INNOCENT J SULLE- My Little Travelling Library
Uhaba wa kupata mada za masomo na kukosekana kwa utamaduni imara wa kujisomea kumechangia kuwepo kwa duru endelevu ya kutokujua kusoma miongoni mwa watoto nchini Tanzania. Watoto wanashindwa kupata vitabu wanavyovipenda kuwepo kwa tabia duni ya kusoma ambayo ni sababu kubwa inayochangia ufanisi duni katika masomo katika shule za msingi nchini. Dhana ya Innocent James ya “Maktaba Yangu Ndogo Inayotembea” inajenga mtandao wa maktaba ya simu, inayowaletea watoto vitabu katika maeneo ya vijijini. Kupitia kazi hii Innocent analenga kuhamasisha utamaduni wa kujisomea miongoni mwa kizazi cha watoto, kuongeza viwango cha kujua kusoma kujitegemea katika kujifunza.
LEKA TINGITANA – eAfya
Leka Tingitana ni mtaalamu wa teknolojia mwenye mapenzi ya kuunda masuluhisho ya kidijitali dhidi ya matatizo katika sekta ya afya. Kupitia kampuni yake ya LX Technological Solutions for Africa, Leka alianzisha jukwaa la mawasiliano ya simu za mkononi la eAfya kusaidia kuunda mtandao wa Jumuia ya Afya ya Wafanyakazi (CHW)
Kuwas wakwanza kusikia kuhusu bidhaa na huduma zetu
Legal Notice
Copyright © 2023 Axian
Privacy Policy